Wizara ya Kilimo na Maendeleo ya Mifugo inaendelea na mazungumzo na Wizara ya Fedha ili kuondoa ushuru wa VAT kwenye mitambo ya uchakataji mazao.
Waziri Peter Kagwe alisema pendekezo hilo litaboresha uwekezaji katika sekta ya kilimo na kuongeza ushindani wa bidhaa za Kenya.
Alitoa maoni hayo wakati wa uzinduzi wa matrekta ya Sonalika na kampuni ya Elgon Kenya katika ukumbi wa KICC jijini Nairobi.
Matrekta tayari hayatozwi ushuru na bei ya Sonalika huanza karibu Sh1.4 milioni. Kampuni hiyo inashirikiana na benki kutoa mikopo ya hadi asilimia 90.