Mashindano ya Afrika
Timu ya miereka ya Kenya imefanya vizuri katika siku ya kwanza ya Mashindano ya Miereka ya Afrika jijini Alexandria, Misri, Jumatatu, kwa kupata medali moja ya fedha na tatu za shaba. Jemimmah Nakhumicha alichukua fedha katika uzani wa kilo 65, huku wachezaji wengine wakipata shaba. Mashindano yanaendelea hadi Mei 2.