Maparachichi
Chama cha Kitaifa cha Biashara na Viwanda Kenya (KNCCI) kimefungua ofisi mpya ya uwakilishi Dubai ili kuimarisha biashara na nchi za Mashariki ya Kati, hasa kwa bidhaa za kilimo kama maparachichi. Hatua hii inatarajiwa kupunguza utapeli na kuchelewa kwa malipo vinavyosababisha hasara kubwa kwa wafanyabiashara wa Kenya.