Marufuku
Ruth chepng'etich apigwa marufuku miaka mitatu na aiu
Mwanariadha wa Kenya Ruth Chepng'etich, mwenye rekodi ya dunia ya marathon, amepigwa marufuku miaka mitatu na Kitengo cha Maadili cha Shirkisho la Riadha Duniani (AIU) baada ya kukubali matumizi ya dawa iliyopigwa marufuku. Sampuli yake iliyochukuliwa Machi 14, 2025 ilionyesha Hydrochlorothiazide (HCTZ) kwa kiwango cha takriban 3,800 ng/mL. Adhabu hiyo imepunguzwa kutoka miaka minne kwa kukubali mapema.