Gilgil
Watu sita wamefariki katika ajali ya mgongano wa gari dogo na basi alfajiri ya Jumamosi katika eneo la Soysambu karibu na Gilgil kwenye barabara kuu ya Nairobi-Nakuru. Ajali hiyo ilihusisha Nissan Wingroad iliyokuwa na wanaume sita na basi la Promise Bus Company. Polisi wamesema abiria zaidi ya 30 wa basi walinusurika bila majeraha.