Kesi ya Ufisadi
Mahakama Kuu ya Kenya imebatilisha hukumu ya awali na kumwacheka huru Bw Moses Lenolkulal, gavana wa zamani wa Kaunti ya Samburu, katika kesi ya ufisadi inayohusiana na kandarasi ya mafuta ya Sh84 milioni. Mahakama ilisema hakuna ushahidi thabiti wa mgongano wa maslahi au uhusiano wa moja kwa moja na biashara hiyo. Pia, wengine wawili waliohusishwa na kesi hiyo wameachiliwa huru.