Uchaguzi wa Kenya
Waziri wa zamani wa Usalama Fred Matiang’i amedai yuko tayari kuunga mkono mgombea mwingine wa urais kutoka Umoja wa Upinzani kwa ajili ya uchaguzi wa 2027, ikiwa atateuliwa kwa njia ya kisayansi na inayokubalika. Hii ni baada ya Jubilee kumteua rasmi kama mgombea wao. Anasema ni muhimu upinzani uwe na mgombea mmoja ili kushinda Rais William Ruto.