Kepsha
Huku Kenya ikijiandaa kuanzisha Shule za Upili chini ya Mfumo wa Elimu Unaotegemea Umilisi (CBE), wadau wa elimu wametaja vipaumbele vya msingi vinavyolenga usawa, ubora na maendeleo. Akizungumza katika kongamano la Kepsha huko Mombasa, Mwenyekiti Bw Fuad Ali Abdalla alisisitiza umuhimu wa miundombinu, uwezo wa walimu na ushirikiano.