Komboa Kenya
Muungano wa upinzani nchini umependekeza kubadilisha jina la Azimio la Umoja kuwa Komboa Kenya Alliance ili kuimarisha nguvu dhidi ya Rais William Ruto kabla ya uchaguzi wa 2027. Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka alithibitisha mazungumzo hayo kwenye Citizen TV. Hatua hiyo inalenga kuepuka changamoto za kisheria na kuharakisha maandalizi ya kampeni.