Mzozo wa ndoa
Mvua kubwa iliyonyesha Nairobi wiki iliyopita imesababisha mzozo mkali kati ya mwanamke na mumewe. Mwanamke huyo, mama wa watoto wanne, alimlaumu mumewe kwa kuchelewa kujenga nyumba ya mawe mashambani ili kuepuka hatari za mafuriko. Alisema, “Sitaki kufa mimi na watoto wangu. Turudi mashambani.”