Utaalamu
Baraza la Madaktari na Wataalamu wa Meno Kenya (KMPDC) limesuta vikali madaktari waliohudhuria mkutano wa Nabii David Owuor na kuthibitisha uponyaji wa wagonjwa kupitia maombi. Mkutano huo ulifanyika Nakuru Desemba 30-31, ambapo madai ya uponyaji wa Ukimwi na magonjwa mengine sugu yalitolewa. Waziri wa Afya Aden Duale ameahidi hatua za kisheria dhidi ya wataalamu hao.