Usimamizi wa Shule
Chama cha Walimu Wakuu wa Shule za Msingi (KEPSHA) na Chama cha Kitaifa cha Walimu (KNUT) vimepinga pendekezo la Tume ya Kuwaajiri Walimu (TSC) la kuwasimishia walimu wa shule za msingi na walimu wa Shule za Sekondari ya Chini (JSS). Viongozi wa vyama hivyo wanasema mpango huo utaanzisha mvutano na kuwa walimu wa JSS wengi hawana tajriba ya kutosha. TSC inasisitiza kuwa mpango huo ni wa kisheria na utasaidia usimamizi bora.