Taita-Taveta
Viongozi wa Kishushe Ranching Cooperative Society Ltd wametoa wito kwa Wizara ya Madini kufafanua taratibu za ridhaa kwa wawekezaji wa madini katika Kaunti ya Taita-Taveta. Wanadai kuwa wawekezaji wanane hawakupata ruhusa kutoka kwa wanachama kama inavyotakiwa na sheria. Wanasisitiza umuhimu wa kufuata taratibu ili kulinda haki za ardhi.