Mila za Kitamaduni
Raila Junior atawazwa kiongozi wa familia ya babake katika sherehe ya kitamaduni
Raila Odinga Junior ametawazwa rasmi kama kiongozi mpya wa familia ya babake, Raila Amolo Odinga, katika sherehe ya kitamaduni iliyofanyika Bondo siku ya Alhamisi, Oktoba 23, 2025. Hafla hiyo, iliyoongozwa na mjomba wake Dkt Oburu Oginga, ilihitimisha kipindi cha maombolezo na kuanzisha uongozi mpya kulingana na mila za jamii ya Waluo. Sherehe ilijumuisha ibada ya kunyoa nywele inayoitwa liedo, ishara ya utakaso na mabadiliko.