Kocha wa Harambee Starlets Beldine Odemba Alhamisi alitaja kikosi cha muda cha wachezaji 29 kitakachoanza maandalizi ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake nchini Morocco.
Wachezaji hao wanatarajiwa kuripoti kambini Jumatatu ijayo. Kikosi hiki kinajumuisha wale waliocheza dhidi ya Zambia na Lesotho mapema mwezi huu pamoja na mastaa wapya kama Lilian Adhiambo na Elizabeth Muteshi.
Starlets zitacheza mechi zao za kundi dhidi ya Morocco Julai 26, Senegal Julai 30 na Algeria Agosti 3. Odemba alisema timu inalenga kufika nusu fainali ili kufungua mlango wa Kombe la Dunia la Wanawake la FIFA 2027 nchini Brazil.
“Kuwakilisha Kenya katika WAFCON ni heshima kubwa. Tunalenga kufika nusu fainali kwa sababu hatua hiyo itatufungulia mlango wa kushiriki,” alisema Odemba.