Waziri wa Fedha John Mbadi amethibitisha kuwa serikali imeidhinisha fedha ili KBC ipeperushe mechi za Kombe la Dunia la 2026 bila malipo.
Mbadi alitoa taarifa hiyo Jumatano tarehe 4 Juni alipokutana na timu ya Gor Mahia jijini Nairobi. Alisema serikali imeshughulikia changamoto za kifedha zilizochelewesha mchakato wa kupata haki za matangazo.
KBC inahitaji takriban Sh150 milioni ili kupata haki hizo. Bila fedha hizo, Wakenya wangehitaji kulipia vituo vya runinga vya Azam TV, New World TV na SuperSport.
Mkurugenzi Mkuu wa KBC Agnes Nguna alithibitisha kuwa makubaliano yanakamilishwa. Mashindano yataanza Juni 11 nchini Marekani, Kanada na Mexico.