Wakazi wa kaunti 13, ikiwemo Nairobi na sehemu za Ukanda wa Bonde la Ufa, Nyanza na Pwani, watapokea mvua ya kiasi na nyingi leo Desemba 29 na kesho Desemba 30, 2025, kulingana na Idara ya Utabiri wa Hali ya Hewa. Naibu Mkurugenzi Kennedy Thiong’o amesema mvua ya kesho itakuwa nyingi lakini itapungua kadri siku inavyoendelea. Hii inafuata mvua iliyoshinda mililita 20 kusini mashariki mnamo Desemba 27.
Idara ya Utabiri wa Hali ya Hewa imetangaza kuwa mvua ya kiasi na nyingi itanyesha kaunti 13 leo na kesho. Kaunti hizo ni Migori, Homa Bay, Kisii, Narok, Kajiado, Makueni, Machakos, Nairobi, Kericho, Bomet, sehemu za kusini mwa Kitui, Taita Taveta na Kwale.
Naibu Mkurugenzi Kennedy Thiong’o alisema, “Mvua ya kesho itakuwa nyingi lakini itapungua jinsi ambavyo siku inavyoendelea.” Aidha, aliongeza kuwa idara yao itaendelea kutathmini hali na kutoa ushauri iwapo hatari zozote zinazonukia, ili msaada utolewe.
Mvua hii inakuja baada ya ile iliyoshuhudiwa kusini mashariki mnamo Desemba 27, ambayo ilishinda mililita 20 ndani ya siku 24. Mvua hiyo ilitarajiwa kupanda hadi zaidi ya mililita 30 ndani ya saa 24 na kuenea maeneo mengine, ikiwemo mashariki, maeneo ya juu ya Bonde la Ufa, Ukanda wa Ziwa Viktoria na sehemu za chini ya ukanda wa Pwani, kutoka Desemba 28 hadi 29.
Asasi za kupambana na majanga ya dharura zimewekwa tahadhari. Mvua hii inatokea baada ya ukame ulioanza kutokana na kukosekana kwa mvua fupi kuanzia Oktoba hadi Desemba.