AGPO
Biashara za wanawake zimenufaika na asilimia 58.3 ya zabuni za serikali chini ya mpango wa AGPO mwaka wa kifedha ulioisha Juni 2025. Takwimu kutoka PPRA zinaonyesha kandarasi zenye thamani ya Sh33.1 bilioni kutoka jumla ya Sh56.8 bilioni. Hata hivyo, washikadau wanasema mchango bado haujafikia malengo ya sheria.