Ukimwi
Kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi, Kaunti ya Nairobi imeipiku Homa Bay na kuongoza kitaifa katika idadi ya maambukizi mapya ya virusi vya HIV. Ripoti ya Baraza la Kitaifa la Kudhibiti Magonjwa ya Kuambikizana (NSDCC) inaonyesha ongezeko la maambukizi kitaifa na idadi ya vifo. Hii imetokea siku moja kabla ya Siku ya Ukimwi Duniani.