Ushahidi
Mtaalamu wa maabara ya serikali, Bi Emilly Okworo, alishuhudia katika mahakama kuu kuwa sampuli za damu kwenye kisu na taulo kutoka chumba cha mauaji ya Starlet Wahu zililingana na DNA yake. Aidha, aligundua shahawa za mshukiwa John Matara kwenye kondomu iliyopatikana hapo. Matara ameshtakiwa kwa mauaji hayo na anazuiliwa katika gereza la Kamiti.