Sacco
Zaidi ya wanachama 5,000 wa Kampuni ya Uwekezaji ya Safaricom (SIC) wakabiliwa na hatari ya kupoteza Sh2 bilioni kutokana na usimamizi mbaya. Ukaguzi maalum ulifichua kuwa sehemu kubwa ya ardhi iliyonunuliwa ni hewa au haiuziki. Mkutano Mkuu wa kila mwaka umeahirishwa huku kampuni ikitarajia hasara ya kwanza kwa miaka mitano.