Zaidi ya wanachama 5,000 wa Kampuni ya Uwekezaji ya Safaricom (SIC) wakabiliwa na hatari ya kupoteza Sh2 bilioni kutokana na usimamizi mbaya. Ukaguzi maalum ulifichua kuwa sehemu kubwa ya ardhi iliyonunuliwa ni hewa au haiuziki. Mkutano Mkuu wa kila mwaka umeahirishwa huku kampuni ikitarajia hasara ya kwanza kwa miaka mitano.
Usimamizi mbaya katika SIC umewahatarisha wanachama zaidi ya 5,000 na hasara inayofikia Sh2 bilioni. Hii imetokana na miaka mingi ya matumizi mabaya ya fedha zilizokusanywa kutoka kwa wanachama na wateja, huku bodi ikiidhinisha ununuzi wa vipande vya ardhi visivyo na thamani.
Shughuli kuu za SIC ni kununua ardhi kuuza kwa faida na kujenga nyumba za kuuza. Sasa kampuni inashikilia ardhi yenye thamani ya Sh1.6 bilioni ambayo ni vigumu kupata au kuuza, baadhi ikiwa kwenye miamba au kuwa na migogoro ya kifamilia.
Ukaguzi ulioagizwa na wanachama mwaka uliopita ulilaumu bodi kwa kuidhinisha ununuzi huo na kupuuza ushauri wa kiufundi. Ripoti ilisema, “Ukaguzi wa kina ulifichua kuwa ardhi yenye thamani ya Sh1,391,834,840 (asilimia 53 ya thamani ya mali yote kwa jumla) inazingirwa na utata kuhusu masuala anuai. Aidha, ardhi yenye thamani ya Sh245 milioni ilijumuisha vipande vya ardhi ambavyo vipo lakini, vinakabiliwa na changamoto zinazovifanya visiuzike.”
Karibu nusu ya ardhi hiyo ilikuwa hewa baada ya maafisa kugeuza gharama za mwaka uliotanguliwa kuwa ununuzi mpya, na kuongeza Sh627 milioni. Wakaguzi walimshutumu mkaguzi wa nje wa 2024 kwa kuvuruga hesabu. Faida za zaidi ya Sh600 milioni kati ya 2021 na 2024 zina maswali ya uhalali.
Kwa mara ya kwanza katika miaka mitano, SIC inatarajia hasara za 2025, na Mkutano Mkuu wa kila Mwaka (AGM) uliopangwa mwezi uliopita ukahirishwa.