Zahara Mohamed, mkazi wa Kaunti ya Lamu, alianza kilimo cha mboga kwenye matairi mnamo 2024 na sasa anapata kati ya Sh15,000 na Sh20,000 kila mwezi.
Bi Mohamed, mwenye umri wa miaka 45 kutoka kijiji cha Kauthara, alikuwa hana kazi ya kulipwa miaka kadhaa iliyopita. Alipata wazo la kutumia matairi kupitia video za TikTok na YouTube.
Anapanda mchicha, spinachi, sukumawiki, hoho na mnavu bila kutumia kemikali. Anatumia mboji na kinyesi cha wanyama wake kama mbolea.
Afisa wa kilimo Lenox Katana alisema njia hii ni rahisi na inafaa maeneo ya mijini. Bi Mohamed husambaza mazao yake sokoni na kwa hoteli za Hindi.