Wakazi wa vijiji 17 vinavyopakana na misitu ya Mangawani, Kaunti ya Kwale, wanaishi kwa hofu kutokana na mfululizo wa mauaji na wizi unaofanywa na wahalifu usiku.
Wakazi wanasema washambuliaji huibuka kati ya saa mbili na saa tatu usiku wakiwa na mapanga na kuwalenga watu wanaorejea nyumbani. Bw Kisilu Mbai, mwenye umri wa miaka 86, alisema kutokujulikana kwa wahusika kunatia hofu kubwa.
Bw Jacob Mwanzia alieleza familia yake ilivunjika moyo baada ya nyanya yake kupatikana ameuawa. Chifu Msaidizi Salim Nzala alisema ripoti za mauaji matatu zimepokelewa tangu Desemba 2025 na zimewasilishwa kwa Idara ya Kuchunguza Uhalifu.
Serikali imeanzisha kituo cha polisi Mangawani na kuongeza doria. Kamanda wa Polisi wa eneo la Pwani Bw Ali Nuno alisema hali ya usalama kwa ujumla imeimarika katika eneo lote.