Wakazi wa Kaunti ya Kilifi wanaendelea kuishi kwa hofu kutokana na makundi ya uhalifu yanayotishia usalama, biashara na utalii. Viongozi wameitisha kikao cha usalama ili kuimarisha operesheni za kudhibiti hali hiyo.
Gavana Gideon Mung’aro aliongoza mkutano huo pamoja na Kamanda wa Polisi wa Ukanda wa Pwani Ali Nuno. Wabunge Owen Baya na Amina Mnyazi walishiriki katika maamuzi ya kuimarisha usalama katika maeneo yaliyoathirika kama Malindi, Gede, Kakuyuni, Mayungu na Mtwapa.
Mung’aro alisema serikali imejitolea kushirikiana na vyombo vya usalama ili kurejesha utulivu. Alisisitiza umuhimu wa kuelimisha wakazi kuhusu jukumu la polisi katika jamii.
Baya alisema mikakati imepangwa ili kukabiliana na wahalifu na kwamba usalama wa wakazi ni kipaumbele. Jumwa alisisitiza kwamba operesheni za usalama zitaendelea bila kukwama na kwamba sheria itachukua mkondo wake dhidi ya wahusika.