Chifu wa eneo la Chakama ameiambia Mahakama ya Mombasa kuwa miili iliyopatikana eneo la Kwa Bi Nzaro ilizikwa kinyume na mila za Wagiriama.
Bw Raymond Charo alisema miili ilizikwa bila nguo wala majeneza na katika makaburi ya kina kifupi. Alieleza kuwa kwa mujibu wa utamaduni wa Wagiriama mazishi hufanyika mchana na mwili huwekwa ndani ya jeneza lenye kina kisichopungua futi sita.
Ushahidi huo ulitolewa katika kesi ya mhubiri Paul Mackenzie na washtakiwa wenzake watano. Wanashtakiwa kwa mauaji ya watu 29 bila kukusudia yaliyotokea mwaka 2025 katika eneo la Kwa Bi Nzaro, Chakama, Kaunti ya Kilifi.
Konstebo wa Polisi Isaiah Barasa na shahidi mwingine walitoa ushahidi kuhusu pikipiki iliyotumika kusafirisha wafuasi hadi eneo hilo.