Rais wa Marekani Donald Trump amedai kuwa vikosi vya usalama wa nchi yake vimefanya shambulio kubwa dhidi ya Venezuela na kumkamata Rais Nicolas Maduro pamoja na mke wake. Taarifa hii aliiwasilisha kupitia mtandao wa Truth Social. Mkutano na wanahabari utafanyika leo Mar-a-Lago.
Rais Donald Trump wa Marekani ametoa taarifa inayodai kuwa nchi yake imefanikiwa kutekeleza operesheni ya shambulio kubwa dhidi ya Venezuela. Kulingana na ujumbe wake kwenye Truth Social, Rais Nicolas Maduro na mke wake wamekamatwa na kusafirishwa nja ya nchi. Operesheni hii ilifanyika kwa ushirikiano na vikosi vya usalama wa Marekani.
Trump alisema: “Amerika imefanikiwa kutekeleza shambulio la kiwango kikubwa dhidi ya Venezuela na kiongozi wake, Rais Nicolas Maduro, pamoja na mke wake, wamekamatwa na kusafirishwa nje ya nchi. Operesheni hii ilifanywa kwa ushirikiano na vikosi vya Usalama za Amerika. Maelezo zaidi yatatolewa baadaye. Kutakuwa na mkutano na wanahabari leo saa 11 asubuhi katika Mar-a-Lago. Asanteni kwa kuzingatia suala hili! Rais DONALD J. TRUMP.”
Hii ni moja ya taarifa zenye mvutano kutoka kwa Trump, ambaye mara nyingi hutumia mitandao ya kijamii kutoa habari za moja kwa moja. Hadi sasa, hakuna uthibitisho rasmi kutoka serikali za Marekani au Venezuela kuhusu tukio hili. Mkutano wa habari utatoa maelezo zaidi kuhusu madai haya.