Uganda imethibitisha kisa kimoja cha Ebola wakati mlipuko unaendelea katika DRC ukisababisha vifo 80. Mgonjwa alikuwa mwanamume mwenye asili ya Congo aliyefariki hospitalini mjini Kampala.
Uganda imethibitisha kisa kimoja cha Ebola. Mgonjwa alikuwa mwanamume mwenye asili ya Congo ambaye aliingia nchini na baadaye alifariki hospitalini mjini Kampala baada ya kuthibitishwa kuwa na Ebola aina ya Bundibugyo.
Wizara ya Afya ya Uganda imesema hatua za ufuatiliaji wa watu aliokutana nao zimeanza ili kuzuia maambukizi zaidi. Mlipuko huo umeendelea katika jimbo la Ituri mashariki mwa DRC na kuathiri maeneo ya Mongwalu na Rwampara ambayo yanajulikana kwa uchimbaji wa dhahabu.
Uganda imeimarisha usalama wake katika mipaka yake na DRC. Africa CDC inaandaa mikutano ya dharura na serikali za DRC, Uganda na Sudan Kusini ili kuimarisha doria mipakani na usambazaji wa vifaa vya afya. WHO inasema Ebola ina kiwango cha vifo cha asilimia 50.