Bunduki iliyoibwa kutoka kwa Jaji Aggrey Muchelule mwaka 2025 imetumiwa katika wizi wa mkahawa wa Chaii Wali Café eneo la Westlands wiki iliyopita.
Jumanne jioni Jaji Muchelule aliiambia polisi kwamba aligundua bunduki yake ya Beretta 92 ilikuwa imeibwa baada ya maafisa wa DCI kumfahamisha kuwa ilipatikana Joska Kaunti ya Machakos.
Bunduki hiyo ilipatikana nyumbani kwa mshukiwa aliyenaswa na kamera za CCTV wakati wa wizi huo. Mshukiwa huyo aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi Jumatatu baada ya kurushiana risasi nao.
Kamanda wa Polisi wa Joska Peter Gichohi alisema mshukiwa alikuwa amejificha eneo hilo tangu tukio la Westlands. DCI ilipata bunduki hiyo pamoja na risasi nne za milimita tisa na simu tatu za mkononi.
Uchunguzi unaonyesha bunduki hiyo ilitumika pia katika wizi Mtwapa Kaunti ya Kilifi Februari mwaka huu. Jaji alisema alipewa risasi 15 alipokabidhiwa silaha hiyo mwaka 2018.