Timu ya Kenya ya vijana wa kike chini ya miaka 17, Junior Starlets, imefuzu kwa Kombe la Dunia baada ya kushinda Afrika Kusini 3-1 katika mechi ya marudiano.
Mechi ilichezwa jana uwanja wa Nyayo jijini Nairobi. Kenya ilishinda kwa jumla ya mabao 5-1 baada ya ushindi wa 2-0 wiki iliyopita mjini Pretoria.
Fainali zitafanyika Morocco kuanzia Oktoba 17 hadi Novemba 8 mwaka huu. Hii ni mara ya pili timu hii kufuzu baada ya ushiriki wa kwanza mwaka 2024.
Gaudencia Maloba alisawazisha bao katika dakika ya 70. Brenda Awuor alifunga kwa penalti na Elizabeth Alizeba Achieng alifunga bao la tatu wakati wa nyongeza.