Wakenya wanaoishi Amerika wanaomboleza kifo cha Titus Wanjala, mwenye umri wa miaka 43, aliyefariki pamoja na River Cropper katika ajali iliyotokea Julai 7.
Gari lililokuwa likiendeshwa na Wanjala lilipoteza mwelekeo na kutumbukia kwenye bwawa mjini Waukee, jimbo la Iowa. Idara ya Polisi ya Waukee ilipokea taarifa saa 10 jioni kuhusu gari lililokuwa limezama kando ya Barabara ya Manchester Boulevard.
Maafisa wa polisi na wazima moto walifanikiwa kuwatoa wawili hao majini lakini walifariki hospitalini. Mkuu wa Polisi Chad McCluskey alisema mioyo yao iko pamoja na familia za waliopoteza maisha.
Majirani katika makazi ya Stratford Crossing Townhomes waliandaa ukumbusho na kesha Jumapili ili kuwaenzi. Mipango ya mazishi inaendelea huku uchunguzi wa ajali ukiendelea.