Mwenyekiti wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Kisiasa amevitaka vyama vya kisiasa kuzingatia sheria na kanuni wakati wa kukabidhi cheti cha usajili kwa chama cha Kenya United Generation jijini Nairobi.
John Lorionokou, mwenyekiti wa ORPP, alisema baadhi ya wanasiasa hutumia vyama vya kisiasa kujinufaisha badala ya kuhudumia wananchi.
Alisisitiza kuwa vyama vina jukumu muhimu katika kuimarisha demokrasia na kwamba viongozi na wanachama wanapaswa kuheshimu sheria na kanuni za vyama vyao.
Vincent Munywoki, kinara wa chama cha KUG, alieleza kuwa usajili wa chama hicho utawapa vijana nafasi ya kushiriki katika siasa na kuleta mabadiliko.
Chama hicho kitajikita katika ajenda za vijana, uwajibikaji na maendeleo ya kijamii na kiuchumi.