Jopo la Kutatua Mizozo ya Ushuru limruhusu aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko kufikia mamilioni yake yaliyozuiliwa katika akaunti za Benki ya Equity tangu 2020. Uamuzi huo ulitolewa Ijumaa na kuamrisha Mamlaka ya Ukusanyaji Ushuru (KRA) iondoe vizuizi. Akaunti hizo sita ni za kati ya 10 zilizo na jumla ya Sh537 milioni.
Jopo la Kutatua Mizozo ya Ushuru lilitoa uamuzi Ijumaa likiamrisha Mamlaka ya Ukusanyaji Ushuru (KRA) iondoe notisi na barua zilizoizuia Mike Sonko kutoa pesa kutoka akaunti zake sita za Benki ya Equity. Akaunti hizo zilikuwa miongoni mwa 10 zilizo na jumla ya Sh537 milioni na zimekuwa zimefungwa tangu Februari 2020 kutokana na tuhuma za ulanguzi wa fedha inayohusishwa na Serikali ya Kaunti ya Nairobi.
Fedha hizo zilizuiliwa awali kwa tuhuma kuwa ni mali haramu iliyopatikana kutoka kaunti hiyo. Hata hivyo, Mahakama Kuu iliondoa amri ya kuhifadhi fedha hizo Oktoba mwaka jana na kuziachilia, kufuatia ombi la Mamlaka ya Kutwaa Mali ya Serikali (ARA).
Mahakama ilisema hakuna msingi wa kisheria wa kurudisha fedha hizo kwa serikali kama ARA ilivyoomba. Uamuzi wa jopo unasema, “Mahakama inaamrisha KRA iondoe notisi na barua ambazo zilizuia Bw Sonko kutoa hela zilizoka kwenye akaunti ya Equity.” Hii inamruhusu Sonko kufikia pesa hizo baada ya miaka sita ya kizuizi.