Soko la Pamoja la Eneo la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) linaendeleza matumizi ya akili mnemba (AI) kusaidia wakulima kuongeza uzalishaji na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Afisa wa Mawasiliano wa Sekretarieti ya COMESA, Leonard Chitunda, alisema wakati wa mafunzo jijini Nairobi kwamba AI inawapa wakulima taarifa za hali ya hewa, afya ya udongo na masoko kupitia simu.
COMESA inatekeleza mpango wa Inclusive Digitalisation for Eastern and Southern Africa unaofadhiliwa na Benki ya Dunia kwa Dola 2.5 bilioni, ambapo Dola 10 milioni zimetengwa kwa sera za pamoja za AI.
Mkurugenzi wa ICT katika Idara ya Serikali ya Biashara nchini Kenya, Timothy Were, alisisitiza hitaji la sheria zinazofanana katika nchi za COMESA ili kuhakikisha usalama wa mifumo ya kidijitali.