Chama cha Social Impact Management Association of Kenya (SIMAK) kimezinduliwa jijini Nairobi ili kuhakikisha haki za wafanyakazi na jamii zinazolindwa katika miradi ya kilimo na maendeleo.
Kaimu Mwenyekiti Profesa Edward Ontita alisema wakati wa uzinduzi kuwa lengo ni kuwepo maafisa wa usimamizi wa kijamii katika kila mradi mkubwa kuanzia hatua ya kupanga.
Alibainisha kuwa mashamba makubwa ya kilimo yanakabiliwa na ukatili wa kijinsia, mishahara duni na mazingira mabaya ya kazi, huku wafanyakazi wakikosa maji safi na uhuru wa kujiunga na vyama vya wafanyakazi.
Dkt Lynett Ochuma kutoka Wizara ya Ulinzi wa Jamii alisema serikali inaandaa sera ya kitaifa itakayowasilishwa bungeni kama mswada ili kuoanisha viwango vya kimataifa na kushughulikia haki za wafanyakazi pamoja na ununuzi wa ardhi kwa haki.