Mamlaka ya Kitaifa ya Usalama wa Kibayolojia (NBA) inaendelea kusimamia ukuzaji wa mimea iliyoboreshwa kijenetiki nchini Kenya ili kusaidia wakulima kupunguza gharama za uzalishaji.
Mkurugenzi Mkuu wa NBA Dkt Ann Karimi alisema mamlaka hiyo inahakikisha bidhaa zote za GMO zinapitia tathmini ya kisayansi kabla ya kuidhinishwa. Jukumu lake si kuhamasisha wala kupinga teknolojia hiyo bali kuhakikisha usalama kwa binadamu mifugo na mazingira.
Pamba ya Bt iliidhinishwa mwaka 2019 na sasa inalimwa katika kaunti mbalimbali. Mahindi ya Bt yamefikia hatua za mwisho za tathmini huku mihogo ya GMO ikiwa imepitia majaribio ya mashambani na bado inachunguzwa.
Changamoto zikiwemo kesi mahakamani na upotoshaji wa habari zimechelewesha uidhinishaji wa baadhi ya bidhaa. NBA imeongeza ukaguzi mipakani na kuimarisha ushirikiano na Kalro pamoja na kampeni za uhamasishaji.