Serikali imeanzisha ujenzi wa makavazi ya heshima kwa marehemu Raila Odinga katika Kang’o ka Jaramogi, Bondo.
Waziri wa Ulinzi Soipan Tuya alisema eneo hilo limefungwa kwa miezi miwili ili kuruhusu ujenzi. Ujenzi huo utafanywa na jeshi na utakamilika kabla ya maadhimisho ya mwaka mmoja tangu kifo cha Raila Odinga.
Hafla ya uzinduzi ilifanyika jana na kuhudhuriwa na Dkt Oburu Oginga, Raila Odinga Junior, Waziri Wycliffe Oparanya na Naibu Gavana Mathews Owili. Familia ilikabidhi eneo hilo kwa serikali leo katika hafla iliyohudhuriwa na Mkuu wa Utumishi wa Umma Felix Koskei na Gavana James Orengo.
Raila Odinga Junior alisema mazungumzo na Dkt Oburu yalijumuisha masuala ya familia na siasa. Kaburi litajengwa karibu na lile la Jaramogi Oginga Odinga aliyefariki Januari 20, 1994.