Waziri wa Fedha John Mbadi anaonekana kujenga nguvu zake za kisiasa katika eneo la Nyanza kufuatia kifo cha Raila Odinga. Kauli zake za hivi karibuni zimemweka katika mvutano na baadhi ya viongozi wa ODM.
Bw Mbadi alisema katika mkutano wa ODM jijini Mombasa mnamo Mei 4 kwamba hatawania kiti chochote cha kisiasa katika uchaguzi wa 2027. Alitetea kauli zake kwa kusema kwamba kila mtu ana hiari ya kuzifasiri jinsi anavyotaka.
Ijumaa iliyopita alitawazwa kuwa mlezi wa Baraza la Wazee wa Luo, tawi la Nairobi. Hatua hiyo inaonekana kama sehemu ya mikakati yake ya kuimarisha nafasi yake kisiasa eneo lote la Nyanza.
Miezi ya hivi karibuni amekuwa akitembelea mazishi na hafla za kisiasa kwa kutumia helikopta ili kujenga uungwaji mkono wa Rais Ruto kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027.