Mwandishi wa zamani wa BBC Ferdinand Omondi amedai kupokea vitisho vya kifo baada ya kuuliza maswali kuhusu mradi wa kiwanda cha mafuta cha Aliko Dangote nchini Lamu.
Omondi, ambaye sasa ni Kiongozi wa Mawasiliano wa Greenpeace Africa kwa Afrika Mashariki na Kusini, alisema vitisho vilianza baada ya kuuliza kuhusu athari za mradi kwa wakazi wa eneo hilo.
Alisema watumiaji wa mitandao walimtishia na kumtukana, huku mmoja akidokeza kuelewa kwa nini serikali huwaalenga watu kama yeye.
Maswali yake yalilenga iwapo jamii zilifahamishwa kuhusu uhamishaji unaowezekana, tathmini ya athari za mazingira, na athari kwa misitu ya mikoko, maeneo ya uvuvi na ardhi ya mababu.
Mradi unatarajiwa kugharimu takriban Ksh2.3 trilioni na kusindika mapipa 700,000 ya mafuta ghafi kwa siku.