Kurejelewa kwa shughuli za uchimbaji mafuta kumeibua tofauti kati ya viongozi katika Turkana Mashariki na Kusini kuhusu ugawaji wa nafasi za kazi na mapato.
Kampuni ya Kawi ya Gulf itasimamia uchimbaji wa mafuta katika Mradi wa South Lokichar baada ya kuchukua nafasi ya Kampuni ya mafuta ya Tullow.
Wakazi wa Aroo wameeleza wasiwasi wao kuhusu kutonufaika, wakitaja kauli za Mbunge Nicholas Ngikor kuhusu nafasi za kazi zitakazopatikana karibu na maeneo ya uchimbaji.
Diwani Samwel Lomodo amesema mwongozo wa maendeleo hauna uwazi kuhusu ajira na ushirikishaji wa umma, huku akishutumu baadhi ya viongozi kwa kuchochea uhasama.
Muungano wa wasomi ukiongozwa na Samwel Ariong na aliyekuwa mbunge Ali Lokiru pia wamelaani upendeleo wa viongozi na ukosefu wa uwazi.