Waziri wa Kawi na Mafuta Opiyo Wandayi alitangaza Ijumaa Juni 5, 2026 kwamba Kenya itaanza kuzalisha mafuta ghafi kutoka kaunti ya Turkana kabla ya mwisho wa mwaka.
Waziri Wandayi alisema mafuta ghafi yatakayozalishwa yatapelekwa ng’ambo kwa ajili ya kusafishwa. Alisema mapato yatatokana na mauzo ya mafuta hayo yatamnufaisha kila Mkenya.
“Kabla ya mwisho wa mwaka huu tutaanza kuzalisha mafuta kutoka Turkana,” alisema katika mahojiano na Radio Jambo. Alibainisha kuwa utekelezaji wa mradi huo umefikia hatua ya uzalishaji.
Kampuni ya Gulf Energy Ltd itachimba mafuta kutoka visima vya Lokichar katika eneo bunge la Turkana Kusini. Kampuni hiyo ilichukua usimamizi wa mradi baada ya kununua mali za kampuni ya Tullow Oil ya Uingereza.