Kutoaminiana na hujuma vilichochea mvutano ndani ya Kitengo cha Ulinzi wa Rais, na kusababisha mapengo ya usalama, imefahamika baada ya tukio la Jumapili iliyopita Kaunti ya Kilifi.
Uchunguzi unaonyesha mazingira ya kazi yalikuwa ya sumu. Maafisa wa chini walilalamikia kunyanyaswa na wakuu wao pamoja na kupendelewa kwa kundi fulani katika kugawa majukumu yenye posho kubwa.
Mgawanyiko kati ya baadhi ya makamanda uliathiri maafisa wa chini. Makundi mawili yalijikuta yakipeleleza wenzao ili kupata makosa yanayoweza kuwafanya wachukuliwe hatua.
Malalamiko mengine yalielekezwa kwa makamanda waliokuwa wakizuia posho za maafisa wanaolinda Rais William Ruto na Ikulu. Maafisa pia walidai upendeleo wa wazi katika kuteua wanaosafiri na rais nje ya nchi.