Mkutano wa ODM uliofanyika Kisumu Jumapili umeonyesha kuwepo kwa mpasuko ndani ya kundi linaloongozwa na Seneta Oburu Oginga.
Viongozi kadhaa wakuu wa chama hawakuhudhuria mkutano huo. Hawa ni pamoja na Naibu Mwenyekiti Otiende Amollo, Millie Odhiambo, Ruth Odinga na Junet Mohamed.
Wafuasi walifurika uwanja wa Kirembe ambapo jamii ya Waluo ilitangaza kuunga mkono Rais Ruto kwa muhula wa pili. Dkt Otiende Amollo alisema alikosa mkutano kutokana na shughuli nyingine Nairobi.
Gavana Anyang Nyong'o alihudhuria na kusema mustakabali wa ODM hautaamuliwa na maeneo ya Luo Nyanza pekee. Duru za chama zinasema Junet Mohamed amekosana na uongozi wa chama.