Ripoti ya Reuters inaeleza kuwa raia saba wa Amerika kutoka shirika la misaada wanaougua Ebola wamewekwa kwenye kituo cha karantini nchini Kenya.
Afisa mkuu wa shirika la Samaritan’s Purse, Franklin Graham, alithibitisha hatua hiyo. Alisema ilitokana na vikwazo vya usafiri vilivyowekwa na utawala wa Rais Donald Trump kwa raia walioambukizwa wanaorejea nyumbani.
Maandamano yalifanyika Nanyuki majuma kadhaa yaliyopita dhidi ya ujenzi wa kituo cha karantini katika kambi ya kijeshi ya Laikipia. Wakaazi walipinga hatua hiyo kwa kuhofia kuenea kwa ugonjwa huo.
Mahakama iliamuru kusitishwa kwa ujenzi huo. Waziri wa Afya Aden Duale aliwasilisha stakabadhi mahakamani kuthibitisha utekelezaji wa amri hiyo baada ya kuitwa kutoa maelezo.
Rais William Ruto alitetea ujenzi wa kituo hicho. Alisema kilikuwa kimoja kati ya vituo vilivyojengwa nchini na kwamba Kenya ina jukumu la kusaidia raia wa Amerika walioambukizwa, huku ujenzi ukifanywa kwa pesa za Amerika.