Mbunge Gregory Meeks amepinga vikali mpango wa Rais Donald Trump wa kujenga kituo cha kutibu wagonjwa wa Ebola nchini Kenya.
Mbunge Gregory Meeks, mwanachama mkuu wa chama cha Democratic katika Kamati ya Masuala ya Kigeni ya Bunge la Amerika, alisema serikali ya Washington ina vituo maalum vya kushughulikia wagonjwa wa Ebola.
Alisema Trump anapaswa kuwaleta raia wake nyumbani badala ya kuhamishia jukumu hilo Kenya. Meeks alilaumu utawala huo kwa kupunguza ufadhili wa afya na kuondoka katika WHO.
Ripoti zinaonyesha maafisa wa Amerika wamefika Kituo cha Jeshi la Anga cha Laikipia. Profesa Kefa Otiso alisema kituo hicho hakitaongeza hatari ya Ebola nchini Kenya.