Kenya itakuwa taifa la kwanza barani Afrika kuandaa Our Ocean Conference kati ya Juni 16 na 18 katika kaunti za Mombasa na Kilifi.
Kongamano la 11 litahusu uhifadhi wa bahari, mabadiliko ya tabianchi na uwekezaji katika uchumi wa baharini. Kaulimbiu yake ni “Bahari Yetu, Urithi Wetu, Mustakabali Wetu.”
Mkurugenzi Mkuu wa East African Wildlife Society Nancy Ogonje alisema litawasukuma wadau kutoa ahadi za utekelezaji na mageuzi ya sera. Alisisitiza umuhimu wake kama jukwaa la kimataifa.
Katibu Mkuu Betsy Njagi alisema sekta ya uchumi wa baharini inachangia asilimia 2.5 ya Pato la Taifa, ikiwa na thamani ya zaidi ya Sh178.8 bilioni kila mwaka. Alisema kuandaa kongamano kutaiweka Kenya kama kitovu cha mijadala ya kimataifa.