Waziri wa Fedha John Mbadi amethibitisha kuwa pendekezo la kuongeza kizingiti cha ushuru wa PAYE kutoka Sh24,000 hadi Sh30,000 bado linazingatiwa. Alitoa ufafanuzi huu wakati wa mkutano wa Mswada wa Fedha 2026 mnamo Mei 11.
Mbadi alisema serikali haijaachana na ahadi yake ya awali ya kutoa unafuu wa ushuru kwa wafanyakazi wanaopata mshahara wa chini ya Sh50,000. Alibainisha kuwa maamuzi yatafanywa kabla ya Juni 30 na mswada huo kupitishwa.
“Kabula mchakato wa ushirikishwaji wa umma umalizike, tutafanya uamuzi. Kabla ya Juni 30 na kabla ya Mswada wa Fedha kupitishwa, serikali inaweza kupendekeza marekebisho ili kuoanisha PAYE na pendekezo letu la awali,” alisema Mbadi.
Alifafanua kuwa simulations zinaonyesha upungufu wa mapato wa takriban Sh35 bilioni kila mwaka ikiwa mabadiliko hayo yatatekelezwa. Pendekezo hilo halikujumuishwa katika Mswada wa Fedha 2026 uliopendekezwa, na hivyo kusababisha wasiwasi miongoni mwa Wakenya.