Viongozi wa UDA kutoka eneo la Mlima Kenya wamemtaka Katibu Mkuu Hassan Omar ajiuzulu mara moja au watawasilisha ombi kwa Rais Ruto kumwondoa.
Viongozi wakiongozwa na Mbunge wa Thika Town Alice Ng'ang'a na Kiambaa John Njuguna Kawanjiku walitoa taarifa pamoja Jumatano Mei 27 wakidai Omar ajiuzulu ndani ya masaa 48. Walisema watawasilisha ombi rasmi ikiwa hatofanya hivyo.
Omar alitoa kauli zenye utata wiki iliyopita wakati wa ziara ya Rais Ruto Pwani akilaumu mgomo wa matatu. Alitoa msamaha baadaye akisema kauli zake zilitafsiriwa vibaya.
Viongozi hao waliunga mkono uchunguzi wa NCIC na kudai mashtaka ya chuki yafuatiliwe. Wengine kama Eric Wamumbi na Veronica Maina walisema wadhifa huo unahitaji mtu anayewaunganisha Wakenya.