Mahali pa kazi ndilo eneo lenye hatari kubwa zaidi ya unyanyasaji wa kingono barani Afrika, kwa mujibu wa utafiti wa GeoPoll uliofanywa nchini Kenya, Nigeria, Afrika Kusini na Misri. Zaidi ya nusu ya wafanyakazi katika nchi hizo wameripoti kukumbana na hali hiyo, na wanawake wakishika nafasi kubwa. Ripoti inaonyesha asilimia 51 ya washiriki wamepitia unyanyasaji huo kazini.
Ripoti mpya ya GeoPoll kuhusu usawa wa kijinsia imebainisha kuwa asilimia 51 ya washiriki katika nchi nne wamewahi kukumbana na unyanyasaji wa kingono kazini. Hii inajumuisha maneno na ishara zisizofaa hadi kuguswa kimwili. Karibu nusu, asilimia 47, ya waliohojiwa wamekiri kupitia aina fulani ya unyanyasaji huo.
Wanawake wanalengwa zaidi, na asilimia 59 wakisema wamepitia hali hiyo ikilinganishwa na asilimia 35 ya wanaume. Pengo kati ya wanaume na wanawake ni asilimia 25. Ripoti inasisitiza kuwa tatizo si la wanawake pekee, kwani mwanaume mmoja kati ya watatu ameripoti unyanyasaji.
Changamoto kuu ni kuto ripotiwa kwa visa vingi. Ingawa mwanamke mmoja kati ya wawili hupitia unyanyasaji, asilimia 30 tu ya visa vinavyoripotiwa. Sababu ni hofu ya kulipiziwa kisasi na kukosa imani kwamba hatua zitachukuliwa.
Mfano ulionekana katika kesi ya Mahakama ya Ajira na Leba Nairobi mwaka jana, ambapo kufutwa kazi kwa wakili kutoka Kituo cha Sheria kuonekana kuwa halali. Mahakama iliamuru fidia ya Sh1.5 milioni baada ya shtumu la unyanyasaji kutoka mfanyakazi wa kiume, akidai aliitwa “baby boy” na “boy lollipop” bila idhini. Mwajiri hakumpa nafasi ya kujitetea.