Mcheshi na mwanaharakati Eric Omondi aliachiliwa Jumatatu na Mahakama ya Milimani Nairobi baada ya kukaa rumande wikendi nzima.
Omondi alikamatwa Ijumaa tarehe 5 Juni 2026 baada ya kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta. Alishtakiwa kwa kuzuia magari kwenye barabara ya Kimathi tarehe 18 Mei 2026 kwa kuweka vibuyu 120 tupu vya plastiki barabarani.
Mawakili wake wakiongozwa na Mbunge Babu Owino walisema mashtaka hayana msingi na walidai kukamatwa kwake kulikiuka Katiba. Polisi walimzuilia Lang'ata bila dhamana hadi Jumatatu.
Mahakama ilimwachilia kwa dhamana ya kibinafsi ya Sh100,000. Kesi itarudi kortini tarehe 22 Juni.